Walisema penzi letu
mwishowe litopunguka.
Walisema jua letu litazama
na giza itatanda.
Walisema rohoni utanitoka.
Walisema penzi letu litafifia,
libaki mazoea.
Waongo hao.
Waongo hawajapata
kuvutiwa na penzi.
Waongo hawajapata
kuridhishwa na penzi.